Advertisement

Responsive Advertisement

PINDA Awataka Vijana kuomba kazi EAC na SADC


WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amewataka wasomi nchini kuondoa hofu ya kutumia fursa zilizo nje ya Tanzania zikiwemo za Jumuiya ya Afrika Mashariki na ile ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) kwa kuomba na kufanya kazi za kujiletea maendeleo.
Akizungumza katika Mahafali ya 48 ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Kampasi ya Dar es Salaam, Pinda alisema inashangaza kuona wananchi wa nchi jirani wakinufaika na nafasi za ajira zilizopo hapa nchini wakati Watanzania wana hofu ya kutafuta ajira katika nchi hizo jirani.
Alisema serikali imeendelea kudumisha ushirikiano na nchi jirani za Afrika Mashariki na SADC na kukubaliana kuondoa vikwazo vya kiuchumi, jamii na kibiashara ili kuwezesha wananchi kunufaika zaidi na fursa zilizopo katika kanda hizo.
“Wakati umefika kwa Watanzania kujenga dhana ya kujiamini na kushiriki kikamilifu katika kuwania nafasi na fursa zilizopo katika jumua hizi. Watanzania tunaweza, jambo la muhimu ni kuamua na kuthubutu.
“Nitumie fursa hii kuwahimiza wahitimu muombe kazi hata zilizo nje ya Tanzania, msifungwe na mipaka, fuateni taratibu kujinufaisha na kulinufaisha Taifa,” alisema.
Akizungumzia umuhimu wa elimu ya biashara, Pinda alisema Serikali ingependa kuona wawekezaji wengi wa Kitanzani wakiwekeza kwenye rasilimali za mbalimbali nchini ikiwamo gesi, madini, kilimo, lakini hilo halitawezekana kama hakutakuwa na wasomi waliobobea kwenye fani hizo.
Alisema kwa kutambua fedha zinazotengwa katika sekta ya elimu kuhusu biashara hazitoshi, alisema Serikali itaendelea kuwekeza katika elimu ya biashara ili wananchi wengi waweze kujiajiri na kuajiriwa katika sekta binafsi hasa biashara.
Katika hatua nyingine, Pinda aliwataka Waziri wa Viwanda na Biashara na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Mandeleo ya makazi kushirikiana kuhakikisha wanawaondoa wavamizi wa eneo la CBE kwa mujibu wa sheria.
Source: Habarileo

Post a Comment

0 Comments