Advertisement

Responsive Advertisement

DOTNATA awachana wanaomponda WEMA


Mjasiriamali na mwigizaji wa sinema za Kibongo, Illuminata Poshi ‘Dotnata’.
MJASIRIAMALI na mwigizaji wa sinema za Kibongo, Illuminata Poshi ‘Dotnata’ ameibuka na kusema anachukizwa na watu wenye kasumba ya kumsema vibaya mwigizaji Wema Sepetu ‘Beutiful Onyinye’, waache.


Akipiga stori na paparazi wetu Dotnata alisema anakerwa sana na watu wanaokuwa na chuki na mwigizaji huyo ambaye yeye anamchukulia kama lulu katika tasnia ya uigizaji.

Mjasiriamali na mwigizaji wa sinema za Kibongo, Illuminata Poshi ‘Dotnata’.

Siwapendi wanaomchukia Wema ambaye mimi huwa namuona kama nyota katika sanaa, wamuache mtoto wa watu afanye kazi zake, si watafute kazi za kufanya kuliko kumuongelea mabaya,” alisema Dotnata pasipo kuwataja majina watu hao.

Post a Comment

0 Comments