Advertisement

Responsive Advertisement

NISHA KUACHIA AUDIO NA VIDEO YA WIMBO WA GUMZO ALIOIMBA NA MZEE MAJUTO


Msanii wa filamu za vichekesho, Salma Jabu aka Nisha anatarajia kuachia wimbo wa "Gumzo" aliyomshirikisha Mzee Majuto. 
Kwa mujibu wa tovuti ya  bongo5 Nisha amesema kuwa ameamua kuachia wimbo huo ili kuwaridhisha mashabiki wake baada ya kumtaka hautoe wimbo huo. 'Kuna kipande cha wimbo nilikiimba kwenye filamu yangu ya Gumzo, sasa mashabiki wamekuwa wakinisumbua kuwa wanakitaka, nikaona kama wanakitaka basi ngoja nitoe wimbo mzima, kama unavyojua mimi na majuto siyo waimbaji ila tumeimba kwajili ya movie, lakini kwa sababu wanaitaka naona bora tuwape ili wafurahi, pia kutokana na mashabiki kuona wanaitaji wimbo wa Gumzo, wiki hii au ijayo tutafanya video yake ,kwaiyo wadau wakae mkao wa kula' Alisema Nisha.

Post a Comment

0 Comments