Advertisement

Responsive Advertisement

BREEEKING....Mwanamuziki mkongwe wa Congo, Tabu Ley Rochereau afariki dunia...!!

Mwanamuziki mkongwe wa Congo, Pascal Tabu Ley Rochereau amefariki dunia leo asubuhi baada ya kulazwa katika hospitali ya nchini ubelgiji.


Kwa mujibu wa mwanae Charles Tabu, Baba yake amefariki kwa uginjwa wa Kiharusi na kisukari.


Naye Nyboma Mwanandido, mwanamiziki mwenzake aishie Pars Ufaransa, amethibitisha kutokea kwa kifo cha Tabuley.


Tabuley alikuwa mgonjwa mahututi katika hospitali hiyo kutokana na kusumbuliwa na Kiharusi alichokipata mwaka 2008.
Kiharusi, yani Stroke kilimfanya awe kwenye kiti cha walemavu tangu wakati huo.
Pamoja na muziki Tbuley aliwaki kuteuliwa kuwa waziri nchini Congo na rais Laurent Kabila mwaka 1997 na baadae pia kuwa mbunge.
Miaka ya mwishoni mwa uhai wake alikuwa akiishi Paris, Ufaransa kabla ya hivi karibuni kupelekwa Ubelgiji kwa matibabu maalumu.
Katika mika yake 46 ya muziki, Tabuley ameshaandika zaidi ya nyimbo 3,000 na kuuza maelfu ya nyimbo.
 

Tabuley, aliyezaliwa November 13, 1940, alikuwa kiongozi wa kundi la Orchestre Afrisa International na mmoja wa wasanii wakubwa katika bara la Afrika katika uimbaji na utunzi wa nyimbo.

Akiwa na mpiga gitaa hodari Dkt Nico Kasanda, Marehemu Tabu Ley alikuwa mwanzilishi wa mtindo wa Soukous, na kuufanya ukubalike kimataifa kwa kuchanganya midundo ya Cuba na Rhumba la Latin Amerika.

Post a Comment

0 Comments