Advertisement

Responsive Advertisement

Baada ya kuachiwa huru Binti aliyehukumiwa Kifo kwa kosa kukubali kuoelewa na Mkristo Akamatwa tena

Meriam Yehya Ibrahim Ishag aliadhibiwa kwa makosa mawili, zinaa na kuasi dini
Mwanamke  Meriam Ibrahim aliyeachiwa huru juzi  baada ya kuhukumiwa kifo kwa kosa la kuolewa na mwanamume mkristo na kukana dini ya kiisilamu amekamatwa tena akiwa na mumewe pamoja na watoto wawili katika uwanja wa ndege mjini Khartoum, Sudan.
 
Meriam amekamatwa na watu takribani 40 waliokuwa wamevalia mavazi ya kiraia ikiwa ni masaa machache  baada ya kuachiwa huru kutokana na uamuzi wa mahakama ya rufaa.
 
Meriam Yehya Ibrahim Ishag aliadhibiwa kwa makosa mawili, zinaa na kuasi dini
Inadaiwa kuwa Meriam aliyejifungulia jela alikuwa anajiandaa kuondoka nchini Sudan pamoja na familia yake.

Post a Comment

0 Comments