Advertisement

Responsive Advertisement

KENYA YASHAMBULIWA TENA, WATU WATANO WAPOTEZA MAISHA USIKU WA KUAMKIA LEO


WATU watano wamepoteza maisha baada ya shambulio lililotokea usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Pandanguo huko Witu wilayani Lamu nchini Kenya kilometa 30 kutoka Mpeketoni yalipotokea mauaji ya watu zaidi ya 60 wiki iliyopita.

Polisi wamesema kuwa waliouawa ni kutoka jamii mbalimbali.

Mkuu wa Polisi nchini Kenya, David Kimaiyo amesema kuwa washambuliaji walivamia kijiji cha Pandanguo na kuua takribani watu watano.

"Bado tunawasaka waliohusika na shambulio hili, habari zaidi zitatolewa baadaye," alisema Kimaiyo.

Post a Comment

0 Comments