Serikali
imewataka madereva wote nchini kuhakikisha wanatumia pembetatu ambazo
zimeruhusiwa kisheria kuwekwa kama ishara pindi magari yao yanapopata
hitilafu barabarani na si kuweka magogo, mawe ama matawi ya miti kama
ishara.
Akijibu
swali la mbunge Hilda Ngoye bungeni Dodoma hii leo, Naibu waziri wa
Mambo ya Ndani ya nchi Mh. Pereira Silima amesema ni kosa kwa dereva
kutumia matawi ya miti kama ishara kuwa gari lake limeharibika huku
akionekana pia akikemea tabia ya madereva hao kuviacha vitu hivyo baada
ya magari yao kutengemaa.
"Kuweka
matawi ama mawe magogo barabarani ni kosa kisheria lakini ni kosa zaidi
pale anapomaliza matengenezo ya gari lake anaacha vitu hivyo bila
kuviondoa, kwa kweli hiyo huweza kupelekea matatizo zaidi ikiwemo ajali"
amesema Waziri huyo.
Amesema
dereva anatakiwa kufuata sheria zinazowataka kuwa na pembetatu ambayo
ni rafiki wa mazingira na si kukata matawi ya miti kwa kuwa yanachafua
barabara na pia yanaharibu mazingira kwani miti hukatwa matawi.
Baada
ya majibu hayo mbunge wa Nkasi Mh. Ally Kessy amelazimika kumpa taarifa
waziri huyo akimtaka kutozuia matumizi ya matawi ya miti kama ishara
kuwa kuna gari limeharibika kwa kuwa matawi hayo husaidia kwa kiasi
kikubwa.
Mh.
Kessy amesema barabara nyingi zina kona na miteremko ama milima mikali
na pindi gari linapoharibika katika mazingira hayo pembetatu haisaidii
na badala yake matawi ya miti yanayowekwa barabarani yatasaidia kwa
kiwango kikubwa huku akisisitiza madereva kuondoa matawi hayo baada ya
magari yao kutengenezwa.
Waziri
Silima ameipokea taarifa hiyo kwa kiasi fulani ingawa hakufafunia ni
vitu gani amevipokea na ambavyo hajavipokea katika taarifa hiyo
0 Comments