Advertisement

Responsive Advertisement

WASHUKIWA 5 WA SHAMBULIO LA LAMU NCHINI KENYA WAUAWA

Vikosi vya Ulinzi vya Kenya KDF vimewapiga risasi watu watano wanaoshukiwa kuhusika na shambulio lililotokea Mpeketoni katika eneo la pwani la Lamu hivi karibuni.
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Kenya imetangaza kuwa, washukiwa hao watano walipigwa risasi na kuuawa wakati walipokuwa wakitoroka, ambapo kumekamatwa pia silaha tatu aina ya AK-47.  
Duru za jeshi la Kenya zimeripoti kuwa, washukiwa hao watano wameuawa katika eneo la msituni, wakati wa operesheni ya pamoja iliyolishirikisha jeshi na vikosi vya usalama.
Katika miezi ya hivi karibuni Kenya imeshuhudia milipuko ya maguruneti na mashambulizi ya silaha.Watu karibu 60 waliuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa katika mashambulio mawili yaliyofanyika hivi karibunikatika eneo la Mpeketoni, huko Lamu nchini Kenya.

Post a Comment

0 Comments