Advertisement

Responsive Advertisement

CCM YAWALALAMIKIA JAJI WARIOBA NA WAJUMBE WA TUME YAKE KUHUSU KAULI ZAO KWA RAIS KIKWETE


Chama cha Mapinduzi -CCM kimedai kuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba Jaji Joseph  Warioba na baadhi ya wajumbe wa tume yake wamemshambulia kwa maneno Mwenyekiti wa chama hicho rais  Jakaya  Kikwete
 
Hatua hiyo imefikiwa kutokana na Mdahalo ulioandaliwa na taasisi ya mwalimu Nyerere ambao umefanyika Jumatatu wiki hii na kwamba kupitia mdahalo huo Jaji Warioba na wajumbe wa tume ya mabadiliko ya katiba  waliitupia lawama CCM na mwenyekiti wake kwamba  hoja zake ni nyepesi, dhaifu na za kutunga.
 
Katibu wa Halmashauri Kuu ya taifa Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye amesema Jaji Warioba na tume yake wameugeuza mchakato wa katiba kama mradi wao binafsi hali inayosababisha wasikubaliane na mtu yeyote anayetaka kutofautiana nao kimawazo
 
Nape Amewataka waache kuchafua mchakato wa katiba unaoendelea bungeni mjini Dododma
 
Aidha  Nape amesema wanayo haki ya kutoa maoni yao kama wanavyoona kwao inafaa kwa kuzingatia katiba ya CCM, Sera na Ilani ya chama hicho.

Post a Comment

0 Comments