Advertisement

Responsive Advertisement

Kiongozi wa vikosi vya Afrika katika Jamhuri ya Afrika Kati (MISCA) asimamishwa

Kiongozi wa vikosi vya Afrika katika Jamhuri ya Afrika Kati (MISCA), Jenerali Jean-Marie Michel Mokoko, amemsimamisha kwa muda kamanda wa kikosi kinachoendesha shughuli zake Boali ambako raia 11 wametoweka wakati wa operessheni ya MISCA mnamo tarehe 24 Machi. Taarifa ya Umoja wa Afrika imesema Jenerali Mokoko ameamua kumsitisha kazi kwa muda kamanda wa kikosi cha Boali na kuwahamisha wanajeshi wote waliokuwepo Boali wakati wa tukio hilo. Hatua hiyo inaangaliwa kama njia mojawapo ya kurahisisha uchunguzi unaoendelea. Uchunguzi huo umeanzishwa kufuatia ripoti ya shirika linalopigania haki za binaadamu la Human Rights Watch inayosema wanajeshi wa Kongo Brazaville wanaotumikia MISCA wanahusika na kutoweka raia hao 11 katika mkoa wa Boali, umbali wa kilomita 80 kaskazini magharibi ya mji mkuu, Bangui.

Post a Comment

0 Comments