mkurugenzi wa Huheso Foundation kahama juma mwesigwa akifungua semina |
Wito umetolewa kwa wananchi wilayani Kahama mkoani shinyanga kuachaa matendo yote yatakayoelekea mtu kupata maambuzi ya virusi vya ukimwi,ikiwa ni sambamba na kuifanyia kazi elimu yanayoipata juu ya ugonjwa huo .
Hayo yamebainishwa leo na mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Huheso Foundation wilayani Kahama Juma Mwesigwa katika semina ya uwezeshwaji iliyofanyika katika ukumbi wa kartasi wilayai humo.
Mwesigwa amesema kuwa sio tu uelewa mdogo bali ni utekelezaji mdogo wa elimu wanayoipata juu ya maswala ya ukimwi kupitia semina mbalimbali wanazozipata.
Kwa upande wake mwezeshaji mkuu katika semina hiyo Dr Kaskile Jumanne amesema kuwa mila potofu,tama ya pesa na ugumu wa maisha ndio changamoto kubwa inayochangia watu wengi hususani vijijini kupata maambukizi.
Dr Jumanne ameongza kuwa ni vyema kuitumia elimu hiyo inayotolewa sambamba na kupima afya afya zao ili kuepukana na maambukizi ya virusi vya ukimwi.
Semina hiyo ya siku moja iliyoandaliwa na shirika la Huheso Foundation imehusisha wajasilia mali 60 a kike wa kituo cha ufundi na ujasilia mali cha Huheso kilichopo wilayani humo.
Muwezeshaji mkuu Dr kaskile jumanne |
mtumishi wa Huheso bw Gabriel akitoa neno kwa washiriki |
mtumishi wa shirika la Huheso jaklin |
tukiwa tunapashwa |
0 Comments