Advertisement

Responsive Advertisement

MABWENI YA SHULE YATEKETEA KWA MOTO MONDULI ARUSHA



WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari Erikisongo wilayani Monduli wamenusurika kifo baada ya vyumba vitano vya mabweni yao kuteketea na moto leo asubuhi.
 
Moto huo ambao inaelezwa chanzo chake ni hitilafu ya umeme ulizuka wakati wanafunzi hao wakiwa darasani. Hakuna mtu yoyote aliyedhurika lakini mali kadhaa za wanafunzi zimeteketea.
 
Kikosi cha Zimamoto kutoka Arusha kilifika wakati tayari mabweni hayo yameshateketea. Mbunge wa Monduli, Mhe. Edward Lowassa ametembelea shule hiyo na kuahidi kuwasafirisha wanafunzi majumbani kwao wakati utaratibu unafanywa kurejesha mabweni hayo katika hali ya kawaida.
 

Post a Comment

0 Comments