Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Lulu Mathias Semagongo ‘Aunty Lulu’
MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Lulu Mathias
Semagongo ‘Aunty Lulu’ amefunguka kuwa ametendwa vya kutosha na marafiki
hivyo kwa sasa hahitaji tena kuwa na rafiki.
Akipiga stori na mwandishi wetu, Aunty Lulu alisema kwa nyakati
tofauti marafiki wamemponza akaachika kwenye uhusiano wa wapenzi wake,
kumgombanisha na watu anaofanya nao kazi na mambo mengi yanayofanana na
hayo hivyo kwa sasa hahitaji marafiki.
“Nimetendwa sana na marafiki, bora niachane nao niishi
kivyanguvyangu, nijitafutie maisha yangu mwenyewe. Sihitaji kabisa
marafiki kwa sasa,” alisema Aunty Lulu.
0 Comments