Advertisement

Responsive Advertisement

MAITI YAKAA MOCHWARI SIKU 34 HADI SASA MKOANI KILIMANJARO


Mgogoro mwingine mkubwa wa kifamilia wa kugombea maiti umeibuka mjini Moshi na kusababisha mwili wa Rosemary Marandu kuhifadhiwa mochwari kwa siku34.
Mwili wa marehemu huyo aliyefariki dunia Septemba4 umehifadhiwa katika hospitali ya KCMC na umekua ukilipiwa shilingi 9,000 kila siku hivyo siku34 gharama yake ni sh306,000.
Mama mzazi wa marehemu alisema mumewe aitwaye Flavian Marandu ndiye anayeshikilia mwili huo hadi sasa bila kutoa sababu yoyote kutokana na kushindwa kuelewana na familia yake.
Hata hivyo baba wa marehemu alisema habari hizo si za kweli na kwamba mkewe anamzushia uongo kwani ameshindwa kuja kupanga taratibu za mazishi.

Post a Comment

0 Comments