Moja ya taarifa ya kushtua na
kuhuzunisha zilizoenea kwenye mitandao ya kijamii, pamoja na watu
kutumiana message ni kuhusu msiba wa aliyekuwa staa wa muziki wa Bongo
Fleva, katika kipindi cha LEO TENA wametafutwa watu wa karibu ili
kuthibitisha taarifa hiyo.
Dada wa marehemu ambaye jina lake ni Rachel amethibitisha kuwa msanii MEZ B amefariki akiwa nyumbani kwao Dodoma.
Mez B aliwahi kuwa kundi moja Chamber Squad na akina Ray C, Noorah na marehemu Albert Mangwea pia.
Msiba uko nyumbani kwao eneo la Kisasa, Dodoma.
millardayo.com itakusogezea taarifa zaidi kutoka msibani Dodoma kila zinaponifikia, #RIP Mez B.
Hii sauti kutoka kwenye Leo Tena @CloudsFM, kasikika NOORAH, TIMBULO na RACHEL ambaye ni dada wa MEZ B.
0 Comments