Diva wa filamu nchini, Wastara Juma ambaye kwa sasa anaripotiwa kuwa
katika mapenzi na mwigizaji mwenzake, Bond Bin Suleiman anadaiwa
kupoteza fahamu mara tu baada ya kupewa taarifa kuwa mpenziwe huyo
amepata mtoto wa nne kwa mwanamke mwingine.
Kwa mujibu wa chanzo makini,
Wastara alipenyezewa ubuyu na mpenzi wa zamani wa Bond, Lulu Semagongo
‘Aunty Lulu’ na kuambiwa kwamba asijishebedue kwani Bond ana mwanamke
mwingine ambaye amejifungua mtoto wa nne hivi karibuni.
“Tunakushangaa unavyojinadi kuwa Bond ni wako na kumpa zawadi ya keki
ya bethidei wakati mwenzako amezaa na mwanamke mmoja baamedi hivi
karibuni. Tena si kwamba mtoto huyo ni wa kwanza, ni wa nne,” kilisema
chanzo hicho kikimnukuu Aunty.
Chanzo hicho kifunguka kuwa, baada
ya kupewa taarifa hizo na Aunty Lulu, alizimia ghafla na kulazwa
hospitali.“Wastara alizimia punde tu baada ya kupewa taarifa hizo,
nasikia walimkimbiza hospitali, akapewa huduma nasikia kidogo sasa
hajambo. Ishu ilikuwa mbaya, Aunty Lulu alimmchana laivu.”
Risasi
lilimtafuta Aunty Lulu ambaye hapo awali alikuwa akilalamikia penzi la
kitumwa la kupigwa mara kwa mara na Bond na hata kufikia mahali na
kushukuru Mungu kwa kutengana kwao na kumuuliza kama habari hizo
zilikuwa na ukweli wowote.
0 Comments