Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
IDARA
ya Uhamiaji katika awamu ya nne ya Rais Jakaya Kikwete imeingiza zaidi
ya Sh.bilioni 474 kwa kipindi cha miaka 10 ambayo imetokana na maboresho
mbalimbali katika idara hiyo.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo Kamishina wa Fedha na Utawala,Piniel Mgonja
amesema kuwa katika awamu ya nne uhamiaji imeweza kufanya kazi ya kisasa
kutokana na mifumo pamoja na ujenzi wa Chuocha kuendeleza maafisa wa
idara hiyo.
Amesema
katika utoaji wa hati ya kusafiria kwa mwezi wanatoa hati 5000 tofauti
na miaka 10 iliyopita ambapo walikuwa wakitoa hati 2500 ambayo ilikuwa
ikitokana na kuchukua muda mrefu wa kuchapa kuliko ivyo sasa zinachapwa
kwa kompyuta.
Mgonja
amesema katika suala la uhamiaji bado changamoto kutokana na kuwa na
uwazi katika mipaka ambapo walifanya uparesheni kuwakamata zaidi ya watu
74 000 kati ya hao watu zaidi 66000 waliondolewa nchini.
Amesema wamezidi kuimarisha katika udhibiti wa njia za mipaka ili nchi isiweze kugubikwa na wahamiaji haramu.
Amesema
katika kipindi kijacho hati kusafiria kwa nchi za Afrika Mashariki
itakuwa moja ya kimataifa ili kuondoa usumbufu kwa wateja wao kutafuta
mara kwa mara kwa hati ya kusafiria kwa Afrika Mashariki
Kamishina wa Fedha na Utawala wa Idara ya Uhamiaji, Piniel
Mgonja akizungumza na waandishi habari juu ya mafanikio ya idara ya uhamiaji
katika awamu ya nne ya Rais Jakaya Kikwete iliyofanyika leo Makao Makuu ya
Idara hiyo Kurasini jijini Dar es Salaam.
Makamishina wa Idara ya Uhamiaji wa kwanza kushoto kutoka mwanzo ,Msemaji wa Idara ya
Uhamiaji,Naibu Kamishina wa Idara ya Uhamiaji ,Abbas Irovya ,Naibu Kamishina
Mussa Lyamba,Mratibu Mwandamizi wa Idara ya Uhamiaji ,Petro Malima ,Mhasibu
Mkuu Karunde ,pamoja na Mkaguzi wa Idara hiyo, Kyando wakimsikiliza Kamishina
wa Fedha na Utawala ,Piniel Mgonja katika mkutano uliofanyika Makao Makuu ya
Idara ya Uhamiaji Kurasini,jijini Dar es Salaam.
0 Comments