Advertisement

Responsive Advertisement

Jeneza la Mandela Lalindwa kwa Ndege maalum za Kivita..!!


*Ndege nne za kivita zatanda angani
*Mkalimani uwanja FNB matatani

JENEZA lililowekwa mwili wa Nelson Mandela, limewekewa vifaa maalumu vya kiusalama vya kulifuatilia wakati likisafirishwa kutoka hospitali ya kijeshi na hata litakaposafirishwa kuelekea kijijini kwake Qunu, kwa ajili ya mazishi.

Helikopta za kijeshi aina ya Oryx, zipatazo nne zikiwa na askari wa miamvuli, zimekuwa zikilifuatilia jeneza hilo katika muda wote wa safari kuelekea Makao Makuu ya Serikali ya Union Buildings.

Jeshi limesema kuwa, helikopta hizo zimewekewa vifaa maalumu vya rada kufuatilia harakati zote za usafirishwaji wa jeneza hilo, mpaka litakapoingia kaburini.

Msemaji wa Jeshi la Afrika Kusini (SANDF), Xolani Mabanga, alipofuatwa kuhojiwa alisema, jeshi halijadili usalama wa vyombo vyake katika vyombo vya habari na kusema kuna haja ya kuangalia mazishi ya Mandela badala ya kujadili usalama.

Mabanga alisema bendera ya Taifa hilo ambalo, limefunika jeneza la Mandela itaondolewa mara tu baada ya mazishi ya Kiserikali kukamilika na kuvalishwa ngozi ya chui, kabla ya kuingizwa kaburini.

“Ngozi ya chui inaonyesha utawala na vile vile tutaweka ngao, ili kuonyesha kuwa mtawala huyo anajilinda na anailinda nchi yake na ni mwana wa mfalme,” alisema Mabanga.

Alisema kuwa Mandela atazikwa pamoja na ng’ombe dume ambaye atachinjwa na kuingizwa pamoja kaburini na vile vile ng’ombe mwingine atachinjwa na nyama yake italiwa, bila kuwekwa chumvi wala kitu chochote

Post a Comment

0 Comments