Advertisement

Responsive Advertisement

MABANGO ALIYOKUTANA NAYO DKT SLAA HUKO KIGOMA YAONE HAPA...!!




viongozi mbalimbali wa CHADEMA wakiwamo Shaban Mambo Mwenyekiti wa chadema Kanda ya magharibi na Rajabu Bujoro Mwenyekiti wa Kasulu wamefungua mkutano hali ikiwa shwari watu wa Kasulu wakionesha ustaarabu wa hali ya juu. Lakini kufumba na kufumbua alipopanda jukwaani Dr Slaa Katibu mkuu wa CHADEMA Taifa kikundi cha watu kiliibuka na mabango mbalimbali huku wakitamka kwa jazba maneno mbalimbali ya kumtaka Zitto na kukejeli upngozi wa juu wa CHADEMA.

Katibu Mkuu ameonesha ustaarabu na demokrasia iliyokomaa alipo ruhusu mabango yasogezwe mbele na kuwataka askari polisi wasiwachukulie hatua wenye mabango. Pia aliwauliza wanakasulu ni wangapi wanataka mkutano uendelee wengi wamenyoosha mikono kutaka mkutano uendelee. Hali si salama sana na nimeacha mpaka naingia mitamboni polisi wanatafuta mbinu mbadala za kuimarisha ulinzi na kuongeza kikosi.


======================

Habari Zaidi
======================

Wakuu,taarifa za kusikitisha ni kwamba Mkutano wa Dr.slaa umevunjika Kasulu,amepigwa mawee na vijana wasiojulikana akiwa Jukwaani,Polisi wanapiga mabomu ya Machozi Muda huu kutawanya watu,haijulikani Slaa ameumizwa kiasi gani lakini polisi wamewahi kumuokoa na kumtorosha kusikojulikana.

hali ni tete wakuu,naomba Munipe muda wa kuwawekea Picha hapa.

Pia awali Mkutano ukiwa unaendelea,Waitara ambaye ni Mkurugenzi wa CHADEMA alitangaza kuwa Matamko na mambo mengine yote ya kumtibulia Dr.slaa yanaratibiwa na Kijana Habib Mchange na Diwani mmoja wa Mwanza(Hakutaja jina).

MODS naamini mnawatu KASULU,wapigieni simu MUDA huu,Mpigieni Tumaini Makene mjue Ukweli huu.naomba muiache Post watu wachangie 



CHANZO: JAMII FORUM

Post a Comment

0 Comments