Advertisement

Responsive Advertisement

WILAYA YA KAHAMA YAADHIMISHA MIAKA 52 YA UHURU KWA KUOTESHA MAHINDI ILI KUDHIBITI NJAA...!!


Mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya akiongoza shughuli ya upandaji wa mahindi katika shamba la halmashauri ya Ushetu wilayani humo


WANANCHI Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga, wametakiwa kuhifadhi mazao ya chakula na kulima kilimo chenye tija kwa kuzingatia ushauri wa serikali na maelekezo kutoka kwa wataalamu wa kilimo ili kunufaika na kilimo chao.
Wito huo umetolewa leo na Mkuu wa wilaya ya Kahama, Benson Mpesya kwenye upandaji wa mahindi katika shamba la mfano kwenye maaadhimisho ya miaka 52 ya uhuru, ambayo Kiwilaya yamefanyika Kitongoji cha Kalaba, kata ya Kisuke. 
Mkuu wa wilaya ya kahama Benson Mpesya Akizungumza na Waandishi wa Habari
Amesema wakulima wengi wamekuwa hawafahamu umuhimu wa kupanda mazao kwa nafasi ili kupata mavuno bora, hivyo halmashauri ya Ushetu imeamua kutoa elimu ya upandaji wa mazao ili wakulima walime kilimo chenye tija.
Mpesya ambaye alikuwa Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, amesema kwa kufanya hivyo mkulima ataweza kupata magunia 25-30 ya mahindi katika hekta moja, na kumtoa katika hali ya umasikini ya kutegemea misaada ya chakula kila mwaka.
Mkuu wa Wilaya akiwa na baadhi ya Wanafunzi wa shule ya msingi Kisuke walioshiriki upandaji huo wa Mahindi
Katika hatua nyingine Mpesya amegawa miti kwa ajili ya kutunza mazingira kwa wananchi, Walimu pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Kisuke, baada ya kushiriki katika zoezi la upandaji wa Mahindi katika hekari moja ya mfano.
Mkuu wa wilaya akikabidhi miche ya miti kwa wananchi na watu wote walioshiriki shughuli hiyo
Awali akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu, Isabella Chilumba amesema lengo la kuotesha mahindi katika maadhimisho hayo ni kuhamasisha kilimo cha kisasa na chenye tija ili kukabiliana na tatizo la Njaa wilayani Kahama.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu, Isabella Chilumba akiongea na Waandishi wa Habari
Chilumba amesema wanatarajia kuendelea na uapandaji huo ili kukamilisha hekari 40 za Mahindi, Alizeti na mazao mengine, na chakula hicho kugawanywa katika shule mbalimbali wilayani kahama katika mpango wa kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula mashuleni.
Maadhimisho hayo kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Uhuru jijini Dar-es-salaam, mgeni rasimi akiwa ni rais Jakaya Kikwete, na kauli mbiu isemayo “Vijana ni Nguzo ya Rasilimali Watu, Tuwaamini, Tuwawezeshe na Tuwatumie kwa Manufaa ya Taifa Letu”.















Post a Comment

0 Comments