Advertisement

Responsive Advertisement

MBUNGE DAVID SILINDE AWAELEZA WANANCHI ALIYOYAFANYA JIMBONI MWAKE TANGU AINGIE MADARAKANI

 Kushoto ni Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Momba Frank Mwakajoka na katikati ni Mbunge David Silinde na kulia ni Katibu mwenezi wa vijana Joseph Kayange.
Na  Saimeni  Mgalula,Mbeya
Mbunge wa Jimbo la Mbozi magharibi Mh. David Silinde (CHADEMA), amewaeleza Wananchi wa jimbo lake maendeleo  aliyoyafanya toka alivyoingia madarakani akiwa na lengo la Wananchi kuendelea kukipenda chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) na kuakikisha Wanachukuwa Madaraka tena 2015.
Hayo aliyasema katika mkutano wa Hadhara ambao ulifanyika katika kituo kidogo cha mabasi Sogea katika mji mdogo wa Tunduma Uliopo jimboni hapa, ambapo alianza kwa kueleza vitu ambavyo amefanya katika jimbo hilo kuwa ni Ujenzi wa shule za msingi sita ambazo na yeye alichangia milioni 300 toka mfukoni kwake kwa ajili ya ujenzi huo mpaka kukamilika
Pia Silinde alisema kuwa baada ya kumaliza ujenzi huo aliomba Madawati  katika Benki ya NMB  akapewa madawati 90 ambayo aligawa madawati  15 kwa kila shule, vilevile kisima ambacho kinatoa maji yenye ujazo wa lita laki moja na sabini kwa ajili ya usambazaji katika mji wa Tunduma
Aliendelea kwa kusema kuwa wamejenga Daraja ambalo liligharimu milioni 48 kutoka Shule ya msingi Majengo Mpaka Msasani na watu wanapita kwa raha tofauti na zamani walikuwa wanasumbuka katika uvukaji.
Pamoja na hayo alisema kuwa alitoa milioni 16 kununua magodoro ambayo aliyasambaza katika vituo vyote vya Afya katika jimbo hilo,
Akijibu swali la Benard Mwashirindi ambalo aliuza "Utatusaidiaje Wanamomba kwa kuwa hatuna Viwanja vya michezo vya kisasa?", Silinde alimjibu kuwa maeneo yote waliokuwa wameyatenga kwa ajili ya viwanja yote yamejengwa na watu ila kuna maeneo mengine ambyo yametengwa ambayo yapo Chapwa ila hawawezi kuanza kujenga kwasababu hawajalipa fidia za wamiliki wa viwanja hivyo.
Akiendelea kutoa ufafanuzi juu ya viwanja hivyo alisema kuwa Halmashauli ya Wilaya ya momba imetenga shilingi 404 milioni kwa ajili ya kilipa fidia ndiyo waendeleze michezo huku akiwahakikishia Wananchi kwa kusema kuwa  suala hilo lilikuwepo toka mda mrefu
Alimalizia kwa kusema kuwa maeneo hayo yametengwa kwa ajili ya Ujenzi wa Halmashauri na wameshaongea na TBA pia katika maeneo hayo baadhi ni kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha ufundi, mahakama, na hospitali kubwa ya Wilaya.

Post a Comment

0 Comments