Advertisement

Responsive Advertisement

Video ya Bomu la Soweto Kuwekwa Hadharani, CHADEMA Kuitisha Mkutano wa Waandishi

Kuna habari japo imewekwa kama tetesi, ina ukweli kwamba CHADEMA wanatarajia kuitisha mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia sakata la bomu la soweto ambalo mpaka hivi leo hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa na serikali. 
 
Inasemekana Mbunge wa Arusha mjini atakuwepo kwenye press hiyo na waandishi wa habari, ambao watapewa video hiyo kama ushahidi ili umma wa watanzania wauone mkanda ambao utatoa taswira chanya kwa wananchi kujua ukweli kuhusu tukio lenyewe.

Habari ambazo zimepatikana ni kwamba CHADEMA wataitisha mkutano na waandishi wa habari kabla ya kurusha video ya bomu la soweto, ambalo lilionyesha wazi jinsi polisi walivyohusika kutekeleza ulipuaji wa bomu.

Mkutano na waandishi wa habari unatarajiwa kuwa siku ya jumapili muda na mahali itatangazwa. 

Tutaendelea ku update kadiri tutakavyokuwa tunapokea taarifa.

Post a Comment

0 Comments