Advertisement

Responsive Advertisement

MAUAJI KAGERA: SOMA WANACHOKIFANYA KIKUNDI HIKI CHA "CHINJACHINJA"

Licha ya kuwepo mauaji ya albino nchini limekuibuka kundi la watu wanao fanya vitendo vya kuchinja watu shingo na kuondoa koromeo kwa watu wa kawaida mkoani Kagera limeongeza hofu kwa wakazi wa wilaya za Bukoba mjini, vijini na Misenyi.

Wakiongea kwa nyakati tofauti wakazi wa mkoa wa Kagera wamesema vitendo vya mauaji ya kikatili ya kuchinja watu shingo na kuondoa baadhi ya viungo vyao vinasikitisha na kuendelea kuleta hofu kubwa kwa wakazi wa mkoa huo ambapo wameogeza kwa kulitaka jeshi la polisi kuendelea kuimarisha ulinzi katika kata ya Kitendaguro, Kibeta na Kagondo na kuhakikisha juhudi za kukomesha vitendo hivyo zinafanyika.
 
Mapema akiongea Kupitia kituo cha  ITV kamanda wa jeshi la polis mkoani Kagera ACP Henri Mwaibambe amesema jeshi la polisi linaendelea na juhudi za kuwasaka wa harifu hao ambapo ameongeza kuwa jeshi hilo sasa linawashikilia watu nane wanaodaiwa kuhusika na matukio ya kuchinja watu wasiokuwa na hatia huku akiwataka wananchi kuwa na subira na kutoa ushirikiana kwa jeshi la polisi ili kwapamoja waweze kudhibiti uharifu huo. 
 
Hivi karibuni yametokea matukio ya watu kuchinjwa wa nakuondolewa baadhi ya viungo vyao katika maeneo ya Kitendaguro na Kibeta Kando na Bugabo Katoma ambapo katika eneo la Rwamishenye wananchi wenye hasila kali walijichukulia sheria mkononi kwa kumpiga mtu hadikufa wakimuhisi kufanya vitendo hivyo.

Post a Comment

0 Comments