Wakati
mgomo wa wafanyabiashara wa kutofungua maduka ukiendelea mjini Songea
mkoani Ruvuma mgomo wa waendesha Daladala uliodumu kwa siku nzima jana
umesitishwa.
Mwenyekiti
wa wasafirishaji wa mkoa wa Ruvuma Bw.Golden Sanga amesema kuwa
wameamua kusitisha mgomo wa Daladala ili kutoa nafasi ya Viongozi
kusikiliza malalamiko ya wafanyabiashara huku mgomo wa kutofungua maduka
ukiendelea.
Kwa
upande wake mwenyekiti wa wafanyabiashara mkoa wa Ruvuma Bw.Isaya
Mbilinyi amesema kuwa madai yao yasiposikilizwa ya kutatuliwa utata wa
mashine za EFDS,ongezeko la kodi kwa asilimia mia moja na kuachiwa kwa
dhamana mwenyekiti wao wa taifa Bw.Johnson Minja mgomo huo utakuwa
endelevu.
Kufuatia
hali hiyo mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bw.Said Mwambungu anawasihi
wafanyabiashara kusitisha mgomo wao kwa kuwa kuendelea kugoma ni
kuwaumiza wasio na hatia bila sababu ya msingi.
Wakati
hayo ya kijiri huko tayari Mwenyekiti wa wafanya biashara Bwana.Johnson
Minja amepewa Dhamana na mahakama Hakimu Mkazi Mkoa wa Dodoma.
0 Comments